Ticker

6/recent/ticker-posts

WAJIBU NA MAJUKUMU YA MKUTANO MKUU WA SERIKALI YA MTAA.



NI kupokea na kujadili taarifa kuhusu: 

•  Miradi inayoendeshwa katika  eneo la Mtaa na maendeleo yake; 

•  Hali ya usalama na ulinzi katika eneo la Mtaa; 

•  Matatizo ya huduma za jamii na hatua zilizochukuliwa; 

•  Maamuzi ya Kamati ya Maendeleo ya Kata au ya Halmashauri ya  Mji,  Manispaa au Jiji kupitia Kamati  ya Maendeleo ya Kata yanayohusu Mtaa; 

•  Maamuzi ya Kamati ya Mtaa na utekelezaji wake;

•  Suala lingine lolote linalohusu  utoaji wa huduma na maendeleo ya kijamii na kiuchumi; 

•  Kumwondoa madarakani  Mwenyekiti wa Mtaa  inapodhihirika kwamba ameshindwa kumudu madaraka  yake kwa kuzingatia sheria.

Sheria Namba 7, 8 na 9 kama  zilivyopitishwa na Bunge mwaka  1982 na kurejewa tena mwaka  1999 na 2000, zinatoa muongozo juu ya uendeshaji na  usimamizi wa Serikali za Mitaa ikiwemo majukumu yake.

Imeandikwa na Mwanasheria

Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm_ )

Wa Jungu la sheria Tanzania

0758218269/0628729934

Chapisha Maoni

0 Maoni