KIFUNGU CHA 141 CHA KANUNI YA ADHABU SURA YA 16 SHERIA ZA TANZANIA.
Mtu yeyote ambaye akiwa ni mwenye nyumba au mkazi wa nyumba anaangalia au anafanya au kusaidia kuangalia au kutunza nyumba hiyo, atamshawishi au anajua msichana wa umri wa chini ya miaka kumi na tano kuja mara kwa mara au kuwepo hapo nyumbani kwa madhumuni ya kujihusisha na ngono na mwanaume yeyote ikiwa ngono hiyo ilikusudiwa kufanywa na mwanaume yeyote, atakuwa ametenda kosa na atawajibika kwa adhabu a miaka mitano.
Isipokuwa kwamba itakuwa ni utetezi wa kutosha chini ya shitaka chini ya kifungu hiki iwapo itabainishwa mbele ya mahakama kwamba alikuwa na sababu ya kutosha kumsababisha aamini na anaamini kwamba msichana huyo alikuwa na umri unaozidi miaka kumi na mbili.
#hakizabinadamu
#haki
#sheria
#jungulasheria
#ijuesheria
0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿