KANUNI NA TARATIBU
Tafadhali soma kwa makini kanuni zetu kabla ya kuanza kutumia Jungu la sheria (Tovuti). Kanuni hizi zitawahusu watembeleaji, wasomaji na watumiaji wa Jungu la sheria Tanzania pekee. Kwa kutumia huduma zetu umekubali kanuni zetu zote na endapo hukubaliani na kanuni hizi sitisha au acha kutumia huduma hii.
KUSITISHA HUDUMA KWAKO
Tunayo haki ya kusitisha mara moja huduma hii bila kukupa taarifa kutokana na sababu yoyote itakayotulazimu sisi kufanya hivyo, pia tunayo haki ya kukusitisha au kukuzuia wewe kutotumia huduma hii kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo sababu za kisheria.
MABADILIKO YA KANUNI
Tunaweza kubadili kanuni zetu wakati wowote ili kukidhi matakwa ya sheria halali, kwahiyo ni jukumu lako wewe msomaji na mtumiaji wa Jungu la sheria kusoma mara kwa mara kanuni hizi pamoja na sera zetu za faragha kuona kama kuna mabadiliko yoyote.
LUGHA CHAFU
Haturuhusu matumizi ya lugha chafu katika kutoa maoni au mrejesho kwetu, lugha ya matusi au maudhi ni kosa kisheria na haikubaliki katika jamii na tamaduni zetu. changia hoja kwa ustaarabu bila kumkwaza mtu mwingine.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿