MADAI
Umewahi
kusikia madai au kesi ya madai? Katika aina za kesi kuna kesi za jinai na
madai, kesi za madai ni zile ambazo zinakuwa hazihusishi ujinai ndani yake ila
hutokana na migogoro au hasara za kibiashara pamoja na kudai fidia kutokana na kusababishiwa
madhara Fulani na mtu mwingine. Mara nyingi kesi hizi huhusisha watu binafsi,
taasisi au serikali dhidi ya taasisi na kinyume chake.
Kesi
hizi za madai mara nyingi huhusiana na mambo ya MIKATABA, NDOA, KAZI, BIASHARA,
ARDHI, MIRATHI, MADHARA, na mengineyo mengi. Kesi hizi hufunguliwa na mtu/watu
binafsi dhidi ya mtu/watu binafsi, taasisi, shirika au serikali na kinyume
chake. Katika kesi hizi mara nyingi lengo huwa ni FIDIA kutokana na madhara au
hasara aliyoipata mwathirika.
MFANO
Kampuni A imeingia katika mkataba
na kampuni B, mkataba huu ni wa ujenzi wa jengo la kampuni B, kampuni B inalipa
fedha nusu za ujenzi wa jengo kwa kampuni A, makubaliano ni kuwa jengo
likamilike kwa mwaka mmoja ndipo zilipwe fedha zilizosalia, baada ya mwaka
mmoja jengo linakamilika lakini kampuni B inashindwa kumalizia kiasi cha fedha
zilizosalia kama deni, KAMPUNI A INAFUNGUA KESI YA MADAI KUDAI DENI
LILILOSALIA.
Katika
kesi za madai, mtu binafsi anaweza kuishtaki SERIKALI endapo kuna vitendo
visivyo vya halali vimefanywa na serikali dhidi ya mtu huyo na kumsababishia
HASARA, ni jambo la kawaida sana kuishtaki serikali inapofanya mambo yanayotia
hasara kwa waathirika. KUISHTAKI SERIKALI SI KUSHINDANA NA SERIKALI, NI HAKI.
ADHABU
KATIKA KESI ZA MADAI
Mara
nyingi adhabu za kesi za madai ni FIDIA, kesi zinazohusu NDOA NA MIRATHI mara
nyingi huhitaji mgawanyo sahihi wa mali. Katika kesi ya madai ni nadra sana
kukutana na hukumu ya kifungo jela japokuwa inawezekana endapo utapewa adhabu
ya kulipa fidia na ukashindwa, adhabu hiyo huhama na kuwa ya kifungo (kwa mtu
binafsi) endapo ni taasisi imeshindwa kulipa fidia, mali zake zinaweza
kushikiliwa na baadae kutaifishwa au kuuzwa kwa lengo la kupata fedha za
kumlipa mwathirika
Jungu Attorneys at Jungu La Sheria Tanzania.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿