Je!! umewahi kusikia "deed poll".
Hii ni nyaraka (document) maalumu inayotumika kubadili au kurekebisha majina katika nyaraka mbalimbali.
Nyaraka hii ni kiapo cha kubadili jina, ambapo mwombaji katika nyaraka hii husema wazi majina ambayo alikuwa akiyatumia awali pamoja na majina mapya anayoyataka.
Nyaraka hii hutengenezwa na mwanasheria na baadae husajiliwa kwa msajili wa nyaraka.
Jungu Attorneys at Jungu La Sheria Tanzania

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿