Ticker

6/recent/ticker-posts

Ni kosa la jinai kupiga picha miili ya marehemu bila ruhusa maalumu.



⚖️ NI KOSA LA JINAI KUPIGA PICHA MIILI YA MAREHEMU BILA RUHUSA MAALUMU 🇹🇿

Kwa mujibu wa Kifungu cha 162 cha Kanuni ya Adhabu [SURA YA 16 R.E. 2022], ni kosa la jinai kupiga au kusambaza picha, video au taswira za miili ya marehemu, waathiriwa wa uhalifu au matukio ya kutisha bila idhini.

🚫 Ni marufuku:

❌ Kupiga picha au video za miili ya marehemu au waathiriwa wa uhalifu.

❌ Kusambaza picha hizo kupitia mitandao ya kijamii au njia nyingine yoyote bila ruhusa.

✅ Inaruhusiwa kupiga picha au video kwa sababu zifuatazo tu:

✔️ Uchunguzi wa kihalifu.

✔️ Shughuli za mazishi kwa miili ya marehemu.

✔️ Sababu nyingine zilizoidhinishwa na polisi au mamlaka husika.

⚠️ Adhabu:

Mtu atakayekiuka kifungu hiki anaweza kutozwa faini ya sio chini ya Tsh 1,000,000 au kifungo cha sio chini ya mwaka mmoja, au vyote kwa pamoja.

🔹 Tafakari kabla ya kupiga na kutuma picha za merehemu mitandaoni!

#SheriaNaHaki ⚖️ #Tanzania 🇹🇿 #UsalamaMtandaoni #HakiZaFaragha

Chapisha Maoni

0 Maoni