Ticker

6/recent/ticker-posts

Kukashifu Imani ya dini ni kosa la jinai.

 


⚖️ KUKASHIFU IMANI YA DINI NI KOSA LA JINAI 🇹🇿

Kwa mujibu wa Kifungu cha 129 cha Kanuni ya Adhabu [SURA YA 16 R.E. 2022], ni kosa la jinai kutusi, kusema maneno, kutoa sauti, au kufanya ishara kwa lengo la kuudhi hisia za mtu kuhusu dini yake.

🚫 Vitendo vinavyoweza kuwa kosa:

❌ Kutamka maneno yanayoudhi hisia za kidini za mtu mwingine.

❌ Kutoa ishara au sauti yenye dhihaka kwa imani ya dini ya mtu mwingine.

❌ Kuweka kitu chochote kinachodhalilisha dini katika mazingira anayoyaona mtu mwenye dini hiyo.

⚠️ Adhabu:

Mtu anayepatikana na hatia anaweza kutozwa faini ya sio chini ya Tsh 3,000,000 au kifungo cha sio chini ya mwaka mmoja, au vyote kwa pamoja.

🔹 Heshimu imani za wengine ili kuepuka mgogoro wa kisheria!

#SheriaNaHaki ⚖️ #Tanzania 🇹🇿 #UhuruWaDini #HeshimaNaAmani

Chapisha Maoni

0 Maoni