Ticker

6/recent/ticker-posts

Makosa kuhusu usajili wa wapiga kura.



⚖️ MAKOSA KUHUSU USAJILI WA WAPIGA KURA 🇹🇿

Kwa mujibu wa Kifungu cha 114 cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Sura no. 1 of 2024, mtu yeyote anayehusika katika udanganyifu wa usajili wa wapiga kura anafanya kosa la jinai.

🚫 Makosa yanayohusiana na usajili wa wapiga kura:

❌ Kutoa taarifa za uongo ili kujisajili au kumsajili mtu mwingine.

❌ Kujisajili mara mbili katika vituo tofauti bila kufuata taratibu.

❌ Kuomba upya kadi ya mpiga kura kwa njia ya udanganyifu.

❌ Kununua, kuuza, kuiba au kuharibu kadi ya mpiga kura kwa lengo la kuzuia mtu kupiga kura au kuongeza kura kwa mgombea fulani.

❌ Kumzuia au kumkwamisha afisa wa uchaguzi katika kutekeleza majukumu yake.

⚠️ Adhabu:

Mtu yeyote atakayepatikana na hatia anaweza kutozwa faini kati ya TZS 100,000 hadi 300,000 au kifungo cha miezi 6 hadi miaka 2, au vyote kwa pamoja.

🔹 Kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki ni wajibu wa kila mmoja. Epuka vitendo vya udanganyifu!

#SheriaNaHaki ⚖️ #Tanzania 🇹🇿 #UchaguziHuru

Chapisha Maoni

0 Maoni