Matumizi ya Lugha ya Matusi, Ugomvi na Vitisho vya Vurugu 🗣️🚫
Kwa mujibu wa Kifungu cha 89 cha Kanuni ya Adhabu, ni kosa la jinai kwa mtu yeyote:
🔹 Kutumia lugha chafu, ya matusi au ya kashfa kwa mtu mwingine kwa namna inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani.
🔹 Kupigana au kusababisha vurugu mahali popote kwa namna inayotishia amani ya watu waliopo.
⚠️ Adhabu: Mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya makosa haya anaweza kufungwa kwa kipindi cha mwaka mmoja.
🛡️ Sheria hii inalenga kulinda jamii dhidi ya vurugu, vitisho na lugha zisizofaa ambazo huvuruga amani ya watu wengine.
#AmaniKwanza#SheriaZaAdhabu #TumiaLughaNzuri #JunguLaSheria 🇹🇿

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿