Hili ni baraza la ardhi lililoanzishwa na kifungu cha tano moja cha sheria ya mahakama za ardhi ambapo baraza hilo huwepo katika kila kijiji hasa vijijini na huwa na wanabaraza wasiopungua saba watatu wakiwa ni wanawake.
Kazi ya baraza hili ni kupokea, kutayarisha na kusikiliza pamoja na kusuluhisha migogoro ya ardhi katika ngazi ya kijiji.
Endapo mgogoro wa ardhi haukufanikiwa kuisha katika baraza hilo, upande ambao haukuridhika unaweza kukata rufaa kwenda baraza la ardhi la kata.
Jungu Attorneys at Jungu La Sheria Tanzania.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿