Ticker

6/recent/ticker-posts

POLISI WANARUHUSIWA KUMHOJI MTUHUMIWA AMBAYE WANAMSHIKILIA KWA KOSA LA JINAI KWA MUDA WA SAA "4" NA NYONGEZA YA SAA "8" TU. Na Johnson Yesaya. LL.B



Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, SURA YA 20 na marekebisho yake yote mpaka 2019. KIFUNGU CHA 50 na 51.


kifungu cha 50(1)(a), kinaruhusu  kumuhoji  mtuhumiwa kwa kipindi  cha  saa  nne  kuanzia  muda  alipochukuliwa kuwa  chini ya  kizuizi  kuhusiana  na  kosa.


Katika  kuhesabu  kipindi kinachoruhusiwa  cha  kumuhoji mtu  ambaye  yuko  kizuizini  kuhusiana  na  kosa, kutahesabika  kuwa  ni sehemu  ya  kipindi  hicho  muda  wowote  ambao  afisa  polisi anayepeleleza  kosa  ameacha  kumuhoji  mtu  au  anasababisha  mtu  huyo kufanya  kitendo chochote  kinachohusiana  na  upelelezi  wa  kosa.


Kipindi cha masaa "4" kinaweza kuongezwa kufikia masaa "12", yaani nyongeza ya masaa "8" endapo kwa sababu za msingi inaonekana mahojiano hayajakamilika. Uongezwaji wa muda wa ziada ni lazima uambatane na maombi kwa hakimu, polisi anayefanya upelelezi kuhusu kesi hiyo anapaswa kuomba kwa hakimu muda wa nyongeza wa mahojiano na kama hakimu ataona inafaa, ataruhusu.


MTU ALIYEHOJIWA KWA ZAIDI YA MASAA KUMI NA MBILI BILA SABABU ZA MSINGI ANAWEZA KUFUNGUA KESI KUDAI FIDIA.


Imeandaliwa na : Jungu la sheria Tanzania.


#ijuesheria

#sheria

#jungulasheria

#mwanasheria

Chapisha Maoni

0 Maoni