KIFUNGU CHA 37(1), (2) na (3) Cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 marekebisho ya 2019.
Pale mtu yeyote anapata hasara ya mali au maumivu ya mwili, au anakufa kutokana na kuchukua hatua au katika harakati za kumsaidia hakimu, afisa polisi au afisa mwingine wa sheria kuzuia utendekaji wa kosa au katika kumkamata mtu ambaye ametenda au anadhaniwa kwa sababu za msingi kuwa ametenda kosa, atatakiwa kupata fidia kwa ajili ya hasara au maumivu na kama atakufa, wategemezi wake au wawakilishi wake kisheria watakuwa na haki ya kupokea fidia ambayo mtu huyo angepokea kama asingekufa.
Kiwango cha fidia kitakacholipwa kitakadiriwa, na mambo mengine yote yahusuyo malipo ya fidia yatashughulikiwa, kulingana na masharti ya sheria iliyopo kwa wakati huo kuhusiana na malipo ya fidia kwa waathirika wa makosa ya Jinai.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿