Ticker

6/recent/ticker-posts

MAKAMPUNI YA SIMU HAYARUHUSIWI KUTOA TAARIFA ZA WATEJA WAO.




SHERIA YA MAWASILIANO YA KIELEKTRONIKI NA POSTA YA MWAKA 2010 KIFUNGU CHA 98 na 99.

Sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na posta ya mwaka 2010, katika kifungu cha 98, kinazitaka Kampuni za mawasiliano, wafanyakazi wa Kampuni na mawakala wa kampuni za huduma za mawasiliano, kutunza na kutozitoa taarifa za wateja wao kwa watu wengine kinyume Cha sheria.

Hakuna MTU anayeruhusiwa kutoa taarifa za mteja isipokuwa tu kama imeruhusiwa na Sheria kufanya hivyo. Taarifa za mteja zinaweza kutolewa endapo zitahitajika na mahakama, maofisa wa usalama, mabaraza ya usuluhishi na kwa Mujibu wa Sheria tu.

Imeandikwa na mwanasheria
Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm_)
Wa Jungu la sheria Tanzania
0758218269/0628729934

Chapisha Maoni

0 Maoni