Ticker

6/recent/ticker-posts

UWE NA AKILI TIMAMU KUINGIA KATIKA MKATABA.



SHERIA YA MIKATABA SURA YA 345 KIFUNGU CHA 11&12.

Kila mtu mwenye umri wa mtu mzima na mwenye akili timamu, ambaye hajazuiwa na sheria yoyote, ana uwezo wa kuingia mkataba.

Makubaliano yanayofanywa na  mtu ambaye hajatangazwa kuwa na uwezo wa kufanya mkataba, hayo kisheria ni batili.

Katika kufanya mkataba, mtu  anasemekana kuwa na akili timamu wakati wa kufanya  mkataba ikiwa ana uwezo wa  kuelewa na kutafakari maslahi  yake katika mkataba husika.

Mtu ambaye mara nyingi anakua na matatizo ya akili, lakini muda mfupi anakuwa timamu, anaweza kufanya mkataba wakati anapokuwa na akili timamu.

Mtu ambaye mara nyingi anakuwa na akili timamu, lakini muda mfupi anakuwa na  matatizo ya akili, hawezi kufanya  mkataba muda anaokuwa na  matatizo ya akili.

Imeandikwa na mwanasheria

Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm_)

Wa Jungu la sheria Tanzania

0758218269/0628729934

Chapisha Maoni

0 Maoni