Kula Njama Kudhoofisha Haki na Kuingilia Mashahidi ⚖️
Kwa mujibu wa Kifungu cha 110 cha Kanuni ya Adhabu, mtu yeyote anayeshirikiana na mwingine kwa lengo la kuharibu mwenendo wa haki au kuingilia mashahidi, anakuwa ametenda kosa la jinai.
🚫 Vitendo vinavyohesabika kama kosa ni pamoja na:
🔹Kula njama na mtu mwingine kumtuhumu mtu kwa kosa ambalo si la kweli.
🔹 Kufanya au kupanga jambo lolote kwa nia ya kuzuia, kuchelewesha au kupotosha mwenendo wa haki.
🔹 Kumshawishi au kumzuia shahidi asiende Mahakamani au asitoe ushahidi kama alivyoitwa kisheria, au hata kujaribu kufanya hivyo.
⚖️ Adhabu:
Kifungo cha hadi miaka mitano jela.
#SheriaZaTanzania #Ushahidi #Haki #JunguLaSheria ⚖️

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿