⚖️ KUMILIKI AU KUTUMIA VIFAA HARAMU VYA MTANDAO — NI KOSA LA JINAI ⚖️
Kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Kimtandao [Sura ya 443 Toleo la 2023], Kifungu cha 10, ni kosa la jinai:
❌ Kumiliki au kutumia kifaa au programu iliyoundwa kwa ajili ya kutenda kosa la mtandao.
❌ Kumiliki au kusambaza nywila (password, access code) au taarifa za kuingilia mfumo wa kompyuta kwa nia ya kutenda kosa.
📌 Adhabu yake ni kali:
Faini isiyopungua Shilingi milioni 10, au
Mara tatu ya faida uliyopata kwa ukubwa wowote.
Au kifungo kisichopungua miaka 3, au vyote kwa pamoja.
📝 Si kila kifaa cha kiteknolojia ni halali—nia na matumizi ndiyo msingi wa kosa.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿