KANUNI YA ADHABU SURA YA 16 KIFUNGU CHA 15 KINASEMA.
Mtu mwenye umri chini ya miaka kumi anachukuliwa kuwa hawezi kuwajibika kijinai kwa kutenda au kutotenda kosa.
Mtu mwenye umri wa chini ya miaka kumi na mbili hatawajibika na kosa lolote la kijinai kwa kutenda au kutotenda jambo, isipokuwa kama itathibitishwa kwamba wakati wa kutenda au kuacha kutenda kitendo hicho alikuwa na uwezo wa kujua kwamba hapaswi kukitenda au kuacha kukitenda.
Mwanaume mwenye umri wa chini ya miaka kumi na mbili atachukuliwa kuwa hawezi kufanya tendo la ndoa.
Imeandikwa na mwanasheria
Johnson Yesaya Mgelwa (@yesayajm_)
Wa Jungu la sheria Tanzania
0758218269/0628729934
0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿