Ticker

6/recent/ticker-posts

Haki miliki. Na Johnson Yesaya. LL.B.



𝐇𝐚𝐤𝐢𝐦𝐢𝐥𝐢𝐤𝐢 (𝑨𝒖 𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 𝒌𝒘𝒂 𝒍𝒖𝒈𝒉𝒂 𝒚𝒂 𝑲𝒊𝒊𝒏𝒈𝒆𝒓𝒆𝒛𝒂), ni utaratibu ulioanzishwa 𝐊𝐢𝐬𝐡𝐞𝐫𝐢𝐚 unaompa mmiliki wa kazi za akili (intellectual property) kama vile 𝒌𝒊𝒕𝒂𝒃𝒖, 𝒔𝒊𝒏𝒆𝒎𝒂, 𝒑𝒊𝒄𝒉𝒂, 𝒘𝒊𝒎𝒃𝒐 𝒂𝒖 𝒕𝒐𝒗𝒖𝒕𝒊, 𝒉𝒂𝒌𝒊 𝒚𝒂 𝒌𝒖𝒂𝒎𝒖𝒍𝒊𝒂 𝒎𝒂𝒕𝒖𝒎𝒊𝒛𝒊 𝒚𝒂𝒌𝒆.

Sheria za hakimiliki zinalenga kulinda maslahi ya watungaji wa kazi za akili dhidi ya matumizi holela ya kazi zao na watu wengine bila kibali kutoka kwa mmiliki wa haki ya kunakili.

Kwa mujibu wa sheria za hakimiliki, kazi ya kiakili inaweza kunakiliwa pekee ikiwa mmiliki anatoa kibali cha kuruhusu kazi yake kunakiliwa. Ikiwa mtu ananakili kazi ya mtu mwingine bila kibali, anakiuka sheria za haki miliki, na inaweza kupelekea mashtaka ya madai au jinai juu yake kutegemeana na sheria za nchi husika.

Mkiukaji wa sheria za haki miliki anaweza kukumbana na hukumu ya kulipa fidia au hata kwenda jela anaposhindwa kulipa fidia. Kwa kawaida, sheria za hakimiliki hulinda haki za watungaji na warithi wao kwa kipindi fulani ambacho kinaweza kuongezwa endepo bado mmiliki wa haki miliki atahitaji kuongeza muda wa umiliki.

Imeandikwa na mwanasheria

Johnson Yesaya Mgelwa @yesayajm_

Wa Jungu la sheria Tanzania.

0758218269/0628729934

Chapisha Maoni

0 Maoni