Hii ni hatua tu katika kesi yoyote ya Jinai na sio uamuzi wa mwisho katika kesi. ( Hatua hii humaliza kesi endapo washtakiwa wakikutwa hawana kesi ya kujibu).
Kwa mujibu wa kifungu cha 293 (2) cha SHERIA YA MWENENDO WA MAKOSA YA JINAI SURA YA 20.
Endapo ushahidi wa upande wa mashtaka umekamilika na mahakama inaona upande wa mashtaka wametoa ushahidi unaoashiria kuwepo jinai, mahakama itatamka kuwa washtakiwa wana "kesi ya kujibu".
Baada ya hapo washtakiwa watafahamishwa haki yao ya kuanza utetezi, na mawakili au washtakiwa wenyewe watataja idadi ya mashahidi watakaokuwa nao na mahakama itapanga siku ya kuanza kusikiliza utetezi.
Imeandikwa na mwanasheria
Johnson Yesaya Mgelwa @yesayajm_
Wa Jungu la sheria Tanzania
0758218269/0628729934
0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿