Kwa mujibu wa kifungu cha 217 cha kanuni ya adhabu sura ya
16, kujaribu kujiua ni kosa la jinai. Kosa hilo linaweza kuhukumiwa kwa adhabu
isiyozidi miaka 5 jela kama inavyoelekezwa na kifungu cha 35 kinachoeleza
adhabu ya jumla kwa makosa ambayo hayajapewa adhabu ya moja kwa moja.
Lakini sheria hiyohiyo inaweka kinga katika kifungu cha 13 na
inatoa msamaha kwa watu wanaofanya makosa wakiwa katika hali ya ugonjwa unaoathiri
akili zao na kufanya wasielewe wanachofanya.
Hivyo basi, endapo mtu amejaribu kujiua akiwa na akili timamu
na ikathibitika hivyo, atahukumiwa kwa adhabu isiyozidi miaka 5, lakini kama amejaribu
kujiua akiwa na hali ya ugonjwa unaoathiri akili yake na kufanya kosa bila kuelewa,
hatakuwa na kosa kisheria kwa kuwa sheria inampa kinga.
Endapo mtu huyo amefikishwa mahakamani, na ikabainika alifanya
kosa akiwa katika hali ya ugonjwa, Basi mtu huyo hana hatia, mahakama inaweza kuamua
mtu huyo kupelekwa katika kituo cha uangalizi wa watu wenye changamoto ya afya ya
akili kwa mujibu wa kifungu cha 219(2)(b) Cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai
sura namba 20.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿