Kwa mujibu wa Ibara ya 20 ya katiba, na kifungu cha 11(4) na (5) cha sheria ya vyama vya siasa, watu wana haki ya kukusanyika pamoja na kutoa maoni au mawazo yao kwa umma ikiwemo kufanya maandamano baada ya kutoa taarifa kwa mkuu wa polisi katika eneo husika ambapo maandamano yatafanyika.
Baada ya taarifa kutolewa, chama cha siasa kinaweza kuendelea na maandamano mpaka itakapotolewa amri nyingine na mkuu wa polisi.

0 Maoni
WEKA MAONI YAKO HAPA.
TAFADHALI USITUMIE LUGHA YA MATUSI AU KUUDHI KWANI NI KOSA KISHERIA.
KARIBU SANA NA ASANTEE.. 🇹🇿